ZAKAH SEHEMU YA 32
Assalam Alaykum Wa RahamatuLLAH Wa Barakatuh
*KUTOA ZAKAH*
========🔹🔷🔹
========
_SEHEMU YA THALATHINI NA MBILI_
*Wanaostahiki Zakaah*
*Wenye Kuzitumikia*
```▶Wanaozitumikia Zakaah ni wale waliopewa jukumu la kuipokea, kuikusanya kutoka kwa matajiri na wenye kazi ya kuihifadhi, waandishi, na wenye kuigawa, wakiwemo wachungaji wa wanyama wa Zakaah.
Ili waweze kupewa katika Mali ya Zakaah, watu hao lazima wawe Waislam, na wasiwe katika wale walioharamishwa kupokea Zakaah katika watu wa Ahlul Bayt ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika Banu 'Abdil-Muttalib ambao tutawataja baadaye.
Katika wanaoitumikia Zakaah, hata akiwa mtu tajiri basi anastahiki kupewa katika mali hiyo, na ikiwa mtu wa aina hiyo amepewa na wakubwa wanaohusika na akawa hana haja nayo mali hiyo, basi aichukuwe na kuwagawia anaowataka au kumnunulia zawadi anayemtaka.
Imepokelewa kuwa ‘Umar bin Al-Khattwaab (Radhwiya Allaahu ‘anhu) alipokuwa akifanya kazi ya kukusanya mali ya Zakaah, Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimpa katika mali hiyo.
‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) akasema:
"Mimi najitolea tu na sina haja ya kulipwa, mpe mwenye kuzihitajia zaidi kuliko mimi".
Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia:
"Alichokupa Allaah katika mali hii bila ya wewe mwenyewe kuiomba, uichukue na uitumie au itolee Swadaqah."
[Al-Bukhaariy na An-Nasaaiy]
Itaendelea In shaa Allah```
*+97433799776*
*RAUDHWATUL ILM*
*UNGANA NASI KUPITIA TELEGRAM BONYEZA LINK IFUATAYO⤵*
https://t.me/joinchat/AAAAAEiWeE_WKW4ORQxRzw
QURAN NA SUNNAH TZ
WHATSAPP NO +255713849566
TEMBELEA KWENYE MITANDAO KWA MASOMO MENGINE ZAIDI👇🏾
websites.
http://qurannasunnahtz.blogspot.com/
Facebook page.
https://m.facebook.com/Quran-na-sunnah-tz-100238655597178/?ref=bookmarks
Instagram.
http://www.instagram.com/qurannasunnah
Whatsapp.
https://chat.whatsapp.com/FfEoBrL4bmr0vbNQhNPKFE
telegram.
https://t.me/joinchat/3WW1yKOS9-MzN2Zk
YouTube
http://m.youtube.com/channel/UC1i0tOe8KZP7L0-rOisIb2A
No comments