ZAKAH SEHEMU YA 33
Assalam Alaykum Wa RahamatuLLAH Wa Barakatuh
*KUTOA ZAKAH*
=======🔹🔷🔹
=======
_SEHEMU YA THALATHINI NA TATU_
*Wenye Kutiwa Nguvu*
```🔥Hawa ni watu wanaopewa katika mali ya Zakaah kwa ajili ya kulainishwa nyoyo zao na kutiwa nguvu kutokana na udhaifu wa nyoyo hizo, na wengine hupewa kwa ajili ya kuwaepusha Waislam na shari zao, au kuwavutia katika kuupenda Uislam na kuupa nguvu.
Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiwapa wakubwa wa makabila ya kiarabu na hasa makabila ya kibedui kwa ajili ya kuwapendekeza katika Uislam.
Imepokelewa kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimpa mtu mmoja aitwae Swafwaan bin Umayyah ngamia wengi sana katika ngamia wa ngawira waliopatikana katika vita vya Hunain, na Safwan huyu alikuwa mkubwa wa kabila lake.
Safwaan alikuwa wakati huo bado hajasilimu, na alipopewa mali hiyo, akarudi kwa watu wake na kuwaambia:
"Enyi watu wangu, ingieni katika dini ya Kiislam, kwani Muhammad anatoa utoaji wa mtu asiyeogopa ufakiri".
(Mwenye kuchunguza, ataona kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiwatendea makabila ya Kibedui tofauti na anavyowatendea watu wa mijini. Alikuwa akiwachukulia kwa akili zao. Na hii ni kwa sababu Mabedui ni watu wagumu sana kufahamu. Hata katika kuuliza masuali, Mabedui walikuwa wakimuuliza Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) masuali na kujibiwa, wakati masuali hayo hayo wangeuliza Maswahaba wanaokaa mjini (Radhwiya Allaahu ‘anhum), basi Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) angekasirika nayo masuali hayo).
Wakati wa ukhalifa wake Abuu Bakr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) alikuwa akiendelea kuwapa watu wa aina hii, lakini ‘Umar bin Al-Khattwaab (Radhwiya Allaahu ‘anhu) siku moja alikataa kutoa, akawaambia:
"Hii Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akikupeni kwa ajili ya kuzizowesha nyoyo zenu na kuzilainisha, lakini sasa Allaah amekwishautukuza Uislam na hatuna haja nanyi tena, mkitaka ingieni katika Uislam, na kama hamtaki basi baina yetu na baina yenu ni panga. Allaah Amesema:
وَقُلِ الْحَقُّ مِن رَّبِّكُمْ فَمَن شَاء فَلْيُؤْمِن وَمَن شَاء فَلْيَكْفُرْ
"Na sema; 'Huu ni ukweli ulotoka kwa Mola wenu, basi anayetaka na aamini na anayetaka na akufuru.”
Al-Kahf: 29
Anasema Sayyid Saabiq katika Fiqhis Sunnah:
"Abu Bakr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) alikubaliana na ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) katika uamuzi wake huo, na hapana hata Sahaba mmoja (Radhwiya Allaahu ‘anhum) aliyepinga. Na hii ni katika Ijtihadi zake ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu), na hata makhalifa waliokuja baada yake, Uthmaan na Aliy (Radhwiya Allaahu ‘anhum) hawakuwapa tena watu wa aina hii katika mali ya Zakaah.
Hata hivyo," anaendela kusema Shaykh Saabiq, "hii haimaanishi kuwa watu wa aina hii wasipewe, na Imaam yeyote yule atakayetawala na akaona kuwa ipo haja ya kuwapa watu wa aina hii, basi atawapa kwa sababu dalili ipo katika Qur-aan na Sunnah.”
Itaendelea In shaa Allah```
*+97433799776*
*RAUDHWATUL ILM*
*UNGANA NASI KUPITIA TELEGRAM BONYEZA LINK IFUATAYO⤵*
https://t.me/joinchat/AAAAAEiWeE_WKW4ORQxRzw
QURAN NA SUNNAH TZ
WHATSAPP NO +255713849566
TEMBELEA KWENYE MITANDAO KWA MASOMO MENGINE ZAIDI👇🏾
websites.
http://qurannasunnahtz.blogspot.com/
Facebook page.
https://m.facebook.com/Quran-na-sunnah-tz-100238655597178/?ref=bookmarks
Instagram.
http://www.instagram.com/qurannasunnah
Whatsapp.
https://chat.whatsapp.com/FfEoBrL4bmr0vbNQhNPKFE
telegram.
https://t.me/joinchat/3WW1yKOS9-MzN2Zk
YouTube
http://m.youtube.com/channel/UC1i0tOe8KZP7L0-rOisIb2A
No comments