NDOA SEHEMU YA 22
*A'ssalam Alaykum Wa RahmatuLLAH Wa Barakaatuh*
🛑. *ADABU ZA MAISHA*
🛑
*YA NDOA - آداب الحياة الزّوجية*
```SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI```
============🔹🔷🔹
============
*8⃣Asimgongee Mwanamme Kumgongea Mke wake Usiku: - ألاّ يطرق الرجل أهله لي*
Imepokewa kutoka kwa Anas bin Maalik:
أنّ النبي صلى الله عليه وسلم كان لا يطرق أهله ليلا كان يدخل غدوة أو عشاء
*“Kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) alikuwa hagongi kwa mkewe usiku, alikuwa akiingia asubuhi sana au ishaa.” (Al-Bukhaariy na Ahmad)*
Kutoka kwa ibn Umar (Radhiya Allahu 'anhuma) anasema kuwa:
وعن ابن عمر أنّ رسول الله صلى الله عليه وسلم نزل العقيق فنهى عن طروق النساء , فعصاه رجلان , فكلاهما رأى ما يكره.
*“Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) alishukia alghaqiiq akakataza kugongewa wanawake, watu wawili wakamuasi (wakenda kugonga kwao) na wote wawili waliona mambo yaliyowachukiza.” (Ahmad)*
Hali kadhalika kutoka kwa 'Abdullaah bin Rawaaha kwamba siku moja alikuwa amerudi kutoka safari akachelewa, na akaona nyumbani kwake pana waka taa, na mke wake anacho kitu pamoja nae, akaamua kuchukua upanga, akasema mkewe: *koma usinisogelee, ni mwanamke Fulani ananisuka, akajiwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) katika hilo na akakataza wanaume kuwagongea milango wake zao usiku. (Ahmad)*
Itaendelea In Shaa Allah
*☎+97433799776*
*NDOA KATIKA UISLAM*
📗〽〽〽〽〽〽〽〽〽📗
QURAN NA SUNNAH TZ
WHATSAPP NO +255713849566
TEMBELEA KWENYE MITANDAO KWA MASOMO MENGINE ZAIDI👇🏾
websites.
http://qurannasunnahtz.blogspot.com/
Facebook page.
https://m.facebook.com/Quran-na-sunnah-tz-100238655597178/?ref=bookmarks
Instagram.
http://www.instagram.com/qurannasunnah
Whatsapp.
https://chat.whatsapp.com/FfEoBrL4bmr0vbNQhNPKFE
telegram.
https://t.me/joinchat/3WW1yKOS9-MzN2Zk
YouTube
http://m.youtube.com/channel/UC1i0tOe8KZP7L0-rOisIb2A
No comments