Header Ads

Header ADS

SWALA YA MGOJWA SEHEMU YA 1

 : ♻Assalam alaykum warahamatullah wabarakatuh


*Swalah ya Mgonjwa*

 📚📚

   📚


1⃣


*VIPI ATASWALI MGONJWA*


↩ kwanza ni wajibu kwa mgonjwa au mtu mwengine kuswali hali amesimama kwani kusimama ni nguzo katika nguzo za swala , Allah anasema : 


📙 حَافِظُوا عَلَى الصَّلَوَاتِ وَالصَّلَاةِ الْوُسْطَىٰ وَقُومُوا لِلَّهِ قَانِتِينَ


Zilindeni Sala, na khasa Sala ya katikati, na simameni kwa ajili ya Allah nanyi ni wenye ku (kunyenyekea).📙


{ البقرة : ٢٣٨ } 


↩ Ama tukija kwa mgonjwa basi ni wajibu pia kwake kusimama , Hata kama ataweza kusimamia kitu kama fimbo au ukuta basi atatakiwa asimame 


{ مجموع فتاوى بن صالح بن العثيمين : ١٥/٢٢٩ } 


↩ Lakini wamekubaliana wanavyuoni kuwa mgonjwa kama Hawezi kusimama basi ataswali kwa kukaa na Hayo yanatokana na kauli ya mtume salallahu alayhi wasallam aliposema : 


📗swali umesimama , kama huwezi , kwa kukaa .... 📗


{ اخرجه البخاري : ١١١٧} 


↩ Lakini swali lakujiuliza utaswali vipi kwa kukaaa ?? 


Mtu atakaa kama vile ambavyo anavyokaa atahiyatu yakwanza (muftarisha) hivi Ndoivyo mtu atakavyokaa kama hawezi kuswali kwa kusimama 


{ فقه السنة للنساء : ١٠٦ } 


↩ kwa ufupi mtu atakaa mkao wowote ambao umewekwa na unakubalika katika sheria lakini lililobora akae mutarabbia (kama wanavyokaa watoto wa madrasa ) katika sehemu za kismamo na akae muftarisha (kile kikao cha attahiyatu ) katika sehemu zote zile za vikao 


{ توضيح الاحكام :٢/١٦٩ } 


↩ Ama ikiwa mgonjwa hawezi kukaa na hawezi kuswali kwa kukaa basi ataswali kwa kulala , na atalalia ubavu wakulia na kuelekea kibla ama kama hawezi basi atalala vile ambavyo ni rahisi kwake 


⬆�Na mgonjwa anaposwali kwa kukaa kutokana na dharura basi swala yake ni sahihi na malipo ni kama ya yule alieswali kwa kusimama 


🎙 Amesema imamu an nawawi : 


📙 wamekubaliana maimamu kuwa asieweza kusimama katika swala za faradhi , aswali hali amekaa , na wala swala hatoilipa , na wala thawabu zake hazitopungua 📗


{ توضيح الاحكام : ٢/١٦٥ } 


↩ Lakini pia ni wajibu kwa mgonjwa arukuu na asujudu 


Lakini Ikitokezea hawezi basi ataashiria kwa kichwa chake , sehemu ya rukuu atainama kidogo na sehemu ya sijda atainama sana kidogo.


Na kama mtu atakuwa ni mgonjwa na hawezi kuashiria kwa kichwa 


Atatumia macho yake kuashiria 


↩ Lakini pia mgonjwa kama anaumwa sanaaa basi anaruhusika kuunganisha swala yani adhuhuri akaswali na alaasiri kabisa



Inaendelea...........



QURAN NA SUNNAH TZ 

WHATSAPP NO +255713849566 


TEMBELEA KWENYE MITANDAO KWA MASOMO MENGINE ZAIDI👇🏾


websites.

http://qurannasunnahtz.blogspot.com/


Facebook page.

https://m.facebook.com/Quran-na-sunnah-tz-100238655597178/?ref=bookmarks


Instagram.

http://www.instagram.com/qurannasunnah


Whatsapp.

https://chat.whatsapp.com/FfEoBrL4bmr0vbNQhNPKFE


telegram.

https://t.me/joinchat/3WW1yKOS9-MzN2Zk


YouTube

http://m.youtube.com/channel/UC1i0tOe8KZP7L0-rOisIb2A



 

No comments

Powered by Blogger.