SWALAH SEHEMU YA 17
*Assalaam Alaykum Wa Rahmatul LLAAHI Wabarakaatuh*
*ALIVYOKUWA AKISOMA*
*(صلى الله عليه وآله وسلم)*
💠 *KTK SWALH MBALMBAL* .💠
SEHEMU YA KUMI NA SABA
1⃣ *Swalah Ya Adhuhuri*
Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akisoma katika Rakaa mbili za mwanzo Suratul-Faatihah na Surah mbili, hurefusha ya kwanza kuliko ya pili.([ *Al-Bukhaairy na Muslim*])
Mara nyingine alikuwa akiirefusha urefu ambao ilikuwa inaweza kufika kuqimiwa kwa Swalah ya Adhuhuri, na aliweza mtu kwenda Al-Baqiy' kukidhi haja yake, [kisha aende nyumbani kwake], kutawadha, kisha aje hali ya kuwa Mjumbe wa ALLAAH (صلى الله عليه وآله وسلم) akiwa bado yuko katika Rakaa ya mwanzo, kwa namna alivyokuwa akiirefusha ([ *Muslim na Al-Bukhaariy katika Juz-u Al-Qiraat (Makala ya Tilaawah)*]).
(Pia) walikuwa wakidhania kwamba alikuwa akifanya hivyo ili watu waweze kuidiriki Rakaa ya mwanzo.([ *Abu Daawuud ikiwa na isnaad Swahiyh na Ibn Khuzaymah (1/165/1).*])
Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akisoma katika kila Rakaa ya hizo Rakaa mbili, kadiri ya Aayah thelathini, kiasi cha kusoma As-Sajdah [32-30] na ikiwemo al-Faatihah. (na kufuatia As-Sajdah [32-30])
Mara nyingine alikuwa akisoma:-
*((وَالسَّمَاء وَالطَّارِقِ))*
*((Naapa kwa mbingu na kinachokuja usiku!))* [At-Twaariq: 86-17], na
*((وَالسَّمَاء ذَاتِ الْبُرُوجِ))*
*((Naapa kwa mbingu yenye Buruji!))* [Al-Buruuj: 85-22], na
*((وَاللَّيْلِ إِذَا يَغْشَى))*
*((Naapa kwa usiku unapo funika!))* [Al-Layl: 92-21], na mfano wa Surah zilizofanana na hizi.([ *Abu Daawuud, At-Tirmidhiy na Ibn Khuzaymah (1/67/2)* ])
Na huenda akasoma
*((إِذَا السَّمَاء انشَقَّتْ))*
*((Itapochanika mbingu)) [Al-Inshiqaaq: 84-25], na mfano wake*. [(Ibn Khuzaymah katika Swahiyh yake (1/67/2)])
Walikuwa wakiweza kuelewa kwamba alikuwa anasoma katika Adhuhuri na Alasiri kutokana na mtikisiko wa ndevu zake.([ *Al-Bukhaariy na Abu Daawuud* )]
In Shaa ALLAAH tutaendelea tena biidhiniLLAAHI.
https://t.me/joinchat/3WW1yKOS9-MzN2Zk
QURAN NA SUNNAH TZ
WHATSAPP NO +255713849566
TEMBELEA KWENYE MITANDAO KWA MASOMO MENGINE ZAIDI👇🏾
websites.
http://qurannasunnahtz.blogspot.com/
Facebook page.
https://m.facebook.com/Quran-na-sunnah-tz-100238655597178/?ref=bookmarks
Instagram.
http://www.instagram.com/qurannasunnah
Whatsapp.
https://chat.whatsapp.com/FfEoBrL4bmr0vbNQhNPKFE
telegram.
https://t.me/joinchat/3WW1yKOS9-MzN2Zk
YouTube
http://m.youtube.com/channel/UC1i0tOe8KZP7L0-rOisIb2A
No comments