Header Ads

Header ADS

SWALA YA EID SEHEMU YA1

 

1⃣ *WAPI INASWALIWA SWALA YA EID*

✍ Sunna nikuswali swala ya eid katika viwanja , yani nje ya msikiti , sehemu ambayo iliokuwa pana na itawakusanyisha waislamu wote ili kudhihirisha utukufu wa Uislamu

✍ Wanaruhusika waislamu wote wanawake , wanaume, watoto, waliokuwa katika siku zao , na waliokuwa tohara wote kuhudhuria katika viwanja panaposwaliwa swala ya eid

✍ Ama waliokuwa katika ada zao wao watu wakiswali hawatoswali Bali wanaruhusika kusikiliza khutba , Kuomba dua na kuleta adhkari mbali mbali

✍ Kuhusiana na kuswali swala ya eid katika viwanja , hii ndio ilikuwa ada ya mtume (salallahu alayhi wasallam na jambo hilo limethibiti katika hadithi nyingi. Miongoni mwa hizo Ni :

🍃 Kutoka kwa Abi said (radhi za Allah ziwe JUU yake ) amesema :

*Alikuwa mtume (salallahu alayhi wasallam) akitoka siku ya fitri na adh-ha katika musalla ....."*

☝ Kutokana na hadithi hio tunajifunza kuwa Ni sunna kuswali eid viwanjani labda kukiwa na dharura basi tutaswali misikitini

*MARRJEO*

الفقه الميسر ( ١.٨)

فقه السنة (١/٣٧٨)

2⃣ *IDADI YA TAKBIRA KATIKA SWALA*

✍ Katika swala ya eid kwa mujibu wa hadithi ya mtume salallahu alayhi wasallam Imamu ataleta Takbira saba katika rakaa ya kwanza

✍ Na katika rakaa ya pili ataleta takbira tano ,

Inaendelea

*+97433799776*
*RAUDHWATUL ILM*

QURAN NA SUNNAH TZ
WHATSAPP NO +255713849566

TEMBELEA KWENYE MITANDAO KWA MASOMO MENGINE ZAIDI👇🏾

websites.
http://qurannasunnahtz.blogspot.com/

Facebook page.
https://m.facebook.com/Quran-na-sunnah-tz-100238655597178/?ref=bookmarks

Instagram.
http://www.instagram.com/qurannasunnah

Whatsapp.
https://chat.whatsapp.com/FfEoBrL4bmr0vbNQhNPKFE

telegram.
https://t.me/joinchat/3WW1yKOS9-MzN2Zk

YouTube
http://m.youtube.com/channel/UC1i0tOe8KZP7L0-rOisIb2A

 

No comments

Powered by Blogger.