Header Ads

Header ADS

TABIA NJEMA SEHEMU 4

 

🌹 *_رياض الصالحين (4 )_*🌹

🌺 *_TABIA NJEMA_* 🌺
▂▂▂▂▂▂▂▂▂▂▂▂▂

🔻 *_KUSHIRIKIANA NA WATU_* 🔻

→ Wengi katika waislamu wa leo , tumeshindwa kujipamba na Tabia hii ya kutangamana / kushirikiana na watu katika mambo mbali mbali yanayotokea

Tumeipa kipao mbele dunia na harakati zake kiasi ambacho kila mda mtu yupo busy na mambo yake au shughuli zake , au biashara zake bila kushiriki chochote kinachotokea katika familia  au jamii anayo ishi

Uislamu umetuhimiza kushirikiana na watu na kutangamana nao vizuri katika :

① Vikao vyenye kheri

② kuzuru na kutembelea wagonjwa

→ Leo hii mtu ndugu yake au jamaa yake anaumwa lakini anashindwa kutumia hata dakika 10 kwenda kumtembelea , badala yake anashuhulika zaidi na harakati au biashara zake

③ Kuhudhuria mazishi

④ kuwafariji wenye shida

⑤ kutowaudhi watu
________

Zimekuja dalili mbali mbali katika Quran na sunna , kubainisha kuwa tunatakiwa tutangamane na watu vizuri

🔻 *_USHAHIDI_* 🔻

(❶) " Na saidianeni katika wema na uchamungu "

(❷) mtume ﷺ ametuamrisha kumzuru mgonjwa , kufata jeneza , kumuombea dua aliepiga chafya , kumfanyia alieapa lile alitakalo , kumnusuru aliedhulumiwa , kumuitikia aliealika na kueneza salamu " Bukhari { 1239 } , Muslim { 2066 }

(❷) " Haki ya muislamu juu ya muislamu ni tano : kurudisha salamu , kumzuru mgonjwa , kufwata jeneza , kuitikia mualiko na kumuombea dua aliepiga chafya "  Bukhari { 1240 } , Muslim { 2162 }

(❸) " wazuruni wagonjwa , mlisheni mwenye njaa na muwache huru mateka "  Bukhari { 6502 }
_________

*_Kwa ufupi_* : muislamu hutakiwi ujitenge au uoneshe ubinafsi , Bali ni katika Tabia njema kushirikiana na watu katika Mas-ala mbali mbali yenye kheri ambayo yanatokea iwe katika familia au jamii ilio kuzunguka

Itaendelea In shaa Allah

_*UNGANA NASI KUPITIA TELEGRAM BONYEZA LINK IFUATAYO⤵*_

https://t.me/joinchat/AAAAAEiWeE_WKW4ORQxRzw

QURAN NA SUNNAH TZ
WHATSAPP NO +255713849566

TEMBELEA KWENYE MITANDAO KWA MASOMO MENGINE ZAIDI👇🏾

websites.
http://qurannasunnahtz.blogspot.com/

Facebook page.
https://m.facebook.com/Quran-na-sunnah-tz-100238655597178/?ref=bookmarks

Instagram.
http://www.instagram.com/qurannasunnah

Whatsapp.
https://chat.whatsapp.com/FfEoBrL4bmr0vbNQhNPKFE

telegram.
https://t.me/joinchat/3WW1yKOS9-MzN2Zk

YouTube
http://m.youtube.com/channel/UC1i0tOe8KZP7L0-rOisIb2A

 

No comments

Powered by Blogger.