Header Ads

Header ADS

SWALAH SEHEMU YA 13

 *Assalaam Alaykum Wa Rahmatul LLAAHI Wabarakaatuh*



             *KUCHANGANYA KWAKE*

              *(صلى الله عليه وآله وسلم)*

                *BAINA YA SURAH*

               *ZINAZOFANANA NA*

💠 *NYINGINEZO KATIKA RAKAA*💠

     ```SEHEMU YA KUMI NA TATU```

============="♦============

 

Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akiunganisha baina ya An-Nadhwaair ((  *"An-Nadhwaair*":--  Ni Surah zilizofanana katika maana. Ni kama zile ambazo zote zina nasaha, maamrisho au visa.)]           

 miongoni mwa Surah za Mufasswal ([ *Mufasswal*, hizi zimekubalika kuwa zinazomalizia Qur-aan mwisho, na mwanzo wake ni Surat Qaaf (Namba 50) kwa rai iliyo sahihi zaidi  ]),  hivyo basi alikuwa akisoma jozi mojawapo za Surah zifuatazo katika Rakaa moja ([ Al-Bukhaary na Muslim )]

 

Ar-Rahmaan (55: 78) ([4]) na An-Najm (53: 62).

Al-Qamar (54: 55) na Al-Haaqqah (69: 52).

At-Twuur (52: 49) na Adh-Dhaariyaat (51: 60).

Al-Waaqi'ah (56: 96) na Al-Qalam (68: 52).

Al-Ma'arij (70:44) na An-Naazi'aat (79:46).

Al-Mutwaffifiyn (83: 36) na 'Abasa (80: 42).

Al-Muddaththir (74: 56) na Al-Muzzammil (73: 20).

Ad-Dahr (76: 31) na Al-Qiyaamah (75: 40).

An-Nabaa (78: 40) na Al-Mursalaat (77: 50).

Ad-Dukhaan (44: 59) na At-Takwiyr (81: 29).

 

Mara nyingine alikuwa akiunganisha baina ya Surah kutoka Sab'at-Twiwaal (Surah Saba ndefu); kama al-Baqarah, an-Nisaa na aal-'Imraan katika Rakaa moja kwenye Swalah ya usiku kama itakavyokuja. Na alikuwa akisema:

*((Swalah bora kabisa ni yenye kisimamo kirefu)).*

 

Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) anaposoma:-

 

*((أَلَيْسَ ذَلِكَ بِقَادِرٍ عَلَى أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَى))*

 

Alaysa dhaalika biqaadirin ‘alaa-an Yuhyiyal Mawtaa

 

*((Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu))*. [Al-Qiyaamah 75: 40)

 

Husema:

 

" *Sub-haanak fabalaa* "

Utukufu ni Wako Ndio hapana shaka

 

Na anaposoma:-


سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى

 

Sabb-hisma Rabbikal A’laa

*((Litakase Jina la Mola wako Mlezi Aliye juu kabisa))*. [Al-A'laa 87: 1)

 

Husema:

*Sub-haana Rabbiyal A’laa*


Ametakasika Mola wangu Aliye juu. 

 

 In Shaa ALLAAH tutaendelea tena . 


*+97433799776*

 


QURAN NA SUNNAH TZ 

WHATSAPP NO +255713849566 


TEMBELEA KWENYE MITANDAO KWA MASOMO MENGINE ZAIDI👇🏾


websites.

http://qurannasunnahtz.blogspot.com/


Facebook page.

https://m.facebook.com/Quran-na-sunnah-tz-100238655597178/?ref=bookmarks


Instagram.

http://www.instagram.com/qurannasunnah


Whatsapp.

https://chat.whatsapp.com/FfEoBrL4bmr0vbNQhNPKFE


telegram.

https://t.me/joinchat/3WW1yKOS9-MzN2Zk


YouTube

http://m.youtube.com/channel/UC1i0tOe8KZP7L0-rOisIb2A



 

No comments

Powered by Blogger.