TABIA NJEMA SEHEMU YA 7
🌹 *_رياض الصالحين(SEH:7)_* 🌹
🌺 *_TABIA NJEMA_* 🌺
▂▂▂▂▂▂▂▂▂▂▂▂▂
🔻 *_KUMTEGEMEA ALLAH_* 🔻
→ Katika Tabia na mwenendo mwema na ndivyo uislamu unavyo tufundisha, tumtegemee Allah ukweli wa kumtegemea katika mambo yetu yote
→ Yoyote anaemtegemea Allah na kumcha kwa kufanya yale alioamrishwa na kuacha yale aliokatazwa basi Allah atamtosheleza na haja zake zote , na ndipo Ibn jubayr aliposema :
*_Kumtegemea Allah ni katika sifa kuu ya imani_*
→ zimekuja dalili mbali mbali katika Quran na sunna kuonesha umuhimu wa kumtegemea Allah katika mambo yetu :
a} iwe wewe ni mwanafunzi unataka kufaulu masomo
b} iwe wewe ni mfanya biashara unataka biashara zako ziende vizuri
c} iwe wewe ni mfanya kazi unataka uwepo sehemu nzuri
d} iwe wewe ni mwanamke unaetaka kuolewa na mume mzuri na mwenye kheri
👆Yote Hayo unatakiwa umtegemee Allah peke yake : ushirikina , kafara , kuroga , ndumba nk yote hayana nafasi kwa anaemtambua na kumuogopa mola wake
♻ *_✾ قال ابن العثيمين رحمه الله_* :
💉 kumtegemea yeye { Allah } katika mambo yako yote , kwani Allah akiwa haja kufanyia wepesi hakuna Atakae kufanyia wepesi { jambo halitokuwa jepesi } , na sababu ya kukufanyia wepesi *_Ni kumtegemea yeye_* ... na utakapomtegema Allah atakutosheleza kwa kila kitu ...
📜الـــمَــصــــــــــدر
🔍 شرح رياض الصالحين { ١/٢٨٤ }
_____
‼ *_Enyi !!!!_* wafanya biashara , wauza maduka , wenye dalala dala , wavuvi , wafanya kazi maofisini ushirikina hauna nafasi katika uislamu Bali tunatakiwa tumtegemee Allah haki ya kumtegemea kama kama anavyotuambia yeye mwenyewe :
۞ *_وَيَرْزُقْهُ مِنْ حَيْثُ لَا يَحْتَسِبُ ۚ وَمَنْ يَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّهِ فَهُوَ حَسْبُهُ ۚ_*
_Na humruzuku kwa jiha { namna} asiyo tazamia. Na anaye mtegemea Allah Yeye humtosha._۞
▂▂▂▂▂
Itaendelea In shaa Allah
_*UNGANA NASI KUPITIA TELEGRAM BONYEZA LINK IFUATAYO⤵*_
https://t.me/joinchat/AAAAAEiWeE_WKW4ORQxRzw
QURAN NA SUNNAH TZ
WHATSAPP NO +255713849566
TEMBELEA KWENYE MITANDAO KWA MASOMO MENGINE ZAIDI👇🏾
websites.
http://qurannasunnahtz.blogspot.com/
Facebook page.
https://m.facebook.com/Quran-na-sunnah-tz-100238655597178/?ref=bookmarks
Instagram.
http://www.instagram.com/qurannasunnah
Whatsapp.
https://chat.whatsapp.com/FfEoBrL4bmr0vbNQhNPKFE
telegram.
https://t.me/joinchat/3WW1yKOS9-MzN2Zk
YouTube
http://m.youtube.com/channel/UC1i0tOe8KZP7L0-rOisIb2A
📚📚
📚
🌹 _*NYONGEZA*_🌹
Katika Suala la kumuomba au kumtegemea Allah kuna watu wa aina tatu :
1) wanamuabudu Allah na kutaka msaada kwa Allah
2) hawataki kumuabudu wala kutaka msaada kwa Allah
👉 Lakini hawa wanapokumbwa na matatizo hujidai kumuomba Allah kwa lengo la kufanikisha haja zao tu
3) Wana muabudu Allah lakini kiuhalisia hawataki msaada wa Allah
👉 waislamu Wengi tumeanguka katika kundi hili
Utamkuta mtu anaingia msikitini , anafunga ramadhani , ametamka shahada nk lakini
a} anapotaka kuuza chipsi au kufungua duka lazima kwanza aende kwa mganga
b} anapotaka kuoa lazima akapige ramli na kuangalia nyota lini na saa ngapi aoe au ambadilishe jina mkewe ili asimtawale
c} anapotaka kupandishwa cheo kazini lazima amroge wajuu yake kwanza ili nafasi aichukue yeye
d} anaamini kuwa bila ya uwepo wa Fulani basi Maisha yake yatakuwa duni { atakuwa masikini }
👆 yoyote ambae yupo katika hili kundi nambari { 3 } basi huyo hayumo katika wale wanaomtegemea Allah katika mambo yao
Kundi bora ni lile nambari { 1 } ambapo wanamuabudu mola wao na kumtegemea.
_____
QURAN NA SUNNAH TZ
WHATSAPP NO +255713849566
TEMBELEA KWENYE MITANDAO KWA MASOMO MENGINE ZAIDI👇🏾
websites.
http://qurannasunnahtz.blogspot.com/
Facebook page.
https://m.facebook.com/Quran-na-sunnah-tz-100238655597178/?ref=bookmarks
Instagram.
http://www.instagram.com/qurannasunnah
Whatsapp.
https://chat.whatsapp.com/FfEoBrL4bmr0vbNQhNPKFE
telegram.
https://t.me/joinchat/3WW1yKOS9-MzN2Zk
YouTube
http://m.youtube.com/channel/UC1i0tOe8KZP7L0-rOisIb2A
No comments