Header Ads

Header ADS

TABIA NJEMA SEHEMU YA 8

 🌹 *_رياض الصالحين (SEH:8)_*  🌹


🌺 *_TABIA NJEMA_* 🌺

▂▂▂▂▂▂▂▂▂▂▂▂▂


🔻 *_KUWA NA SUBIRA_* 🔻



→ Mengi maovu tunayafanya kwa sababu yaku kosa subira na uvumilivu wakati uislamu unahimiza tuwe na subira katika harakati zetu zote za kimaisha 



🎒 Subira imegawika katika sehemu kuu tatu : 


① Subira katika utiifu { kumtii Allah } 


② Subira katika kujihifadhi na kujilinda na yalioharamu 


③ Subira katika lile alilokukadira Allah 

▂▂▂▂▂



*_LA KWANZA_* : 


→ Mtu anatakiwa awe na subra katika kumtii Allah : kwani katika kutekeleza maamrisho mtu anaweza akaona uzito katika nafsi na mwili wake : Lakini anatakiwa mtu ajitahid na afanye yote ambayo mola wake amemuamrisha 



*_LA PILI_* 


→ Pia mtu anatakiwa awe na Subira kwa kujiepusha na yale yote ambayo Allah amekataza : kwani nafsi siku zote inaamrisha maovu Kwaio mtu anatakiwa awe mvumilivu na asifuate yale ambayo nafsi inamuamrisha kama vile uongo , kufanya hadaa katika biashara , wizi , kufanya uzinifu , kunywa pombe na mengineyo 



*_LA TATU_* 


→ Mtu anatakiwa awe na subra kwa lile ambalo Allah amemkadiria : mfano mtu amefukuzwa kazi , amefiliwa na anaempenda , amepatwa na maradhi , mali yake imepotea au kuharibika nk 


📜الـــمَــصــــــــــدر

🔍 شرح رياض الصالحين { ١/٧٨ } 

•┈•✾•┈•┈••✾


Zimekuja dalili mbali katika katika Quran kuhimiza suala zima lakuwa na Subira kama Allah anavyotubainishia 



(❶)  " Enyi mlio amini! Subirini, na shindaneni kusubiri, na kuweni macho, na mcheni Allah, ili mpate kufanikiwa." { 3:200}



(❷) " Hapana shaka tutakujaribuni kwa chembe ya khofu, na njaa, na upungufu wa mali na watu na matunda. Na wabashirie wanao subiri,"  { 2:155 }



(❸) "  Hakika wenye subira watapewa ujira wao bila ya hisabu. " { 39:10 } 

___



💉 Kwaio Tunapaswa kuwa na Subira kwa kufanya yote yalio mema na kuacha yote yalio maovu , hakika Allah amewaandalia wote wenye Subira malipo makubwa na mazuri 


Itaendelea In shaa Allah


_*UNGANA NASI KUPITIA TELEGRAM BONYEZA LINK IFUATAYO⤵*_


https://t.me/joinchat/AAAAAEiWeE_WKW4ORQxRzw



QURAN NA SUNNAH TZ 

WHATSAPP NO +255713849566 


TEMBELEA KWENYE MITANDAO KWA MASOMO MENGINE ZAIDI👇🏾


websites.

http://qurannasunnahtz.blogspot.com/


Facebook page.

https://m.facebook.com/Quran-na-sunnah-tz-100238655597178/?ref=bookmarks


Instagram.

http://www.instagram.com/qurannasunnah


Whatsapp.

https://chat.whatsapp.com/FfEoBrL4bmr0vbNQhNPKFE


telegram.

https://t.me/joinchat/3WW1yKOS9-MzN2Zk


YouTube

http://m.youtube.com/channel/UC1i0tOe8KZP7L0-rOisIb2A



 📚📚

    📚


🌹 _*NYONGEZA*_🌹


Siku zote muumini na muislamu wa kweli anatakiwa awe na dhana njema kwa mola wake kwa chochote /lolote ambalo litamtokezea kama mtume ﷺ anavyotubainishia

 


🔻 *_Ajabu ya jambo la muumini , hakika mambo yake yote ni kheri , wala hakuna Anaepata hilo isipokuwa muumini peke : Akipatwa na furaha hushukuru ikawa ni kheri kwake , na akipatwa na madhara husubiri ikawa { pia } ni kheri kwake_* 🔺 Muslim { 2999 } 



💉 Muislamu anapopatwa na msiba , matatizo , majanga , balaa na kila aina ya msiba basi mambo yafutayo anatakiwa ashikamane nayo : 



(❶) *_Akae kimya_* 


Na huku kukaa kimya au kunyamazia kupo kwa aina mbili : 


a} kwa moyo : yani asiwe na hasira na mola wake pia asiwe na dhana mbaya kwa Allah , wala asijetia moyo mwake kuwa Allah hampendi au amemdhulumu nk 


b} kwa ulimi : hii mtu anatakiwa baada ya kupatwa na msiba au matatizo asitoe Maneno machafu , au asiombe maangamizo 


Mfano Ahhhhh ndo nishafukuzwa kazi bora ningekufa au bora ningeondoka duniani 


Au baba ndo usha fariki hakuna wa kunisaidia bora ningetangulia Mim au tungeondoka pamoja nk 


❌ Aina hizo zote hazitakiwi pindi mtu anapokumbwa na 

 au matatizo 



(❷) *_Awe na Subira_* 


Ukikumbwa na tatizo basi unatakiwa uwe mvumilivu na Allah atakupa mbadala wake ambacho kina kheri zaidi 



(❸) *_Uridhie kile ambacho Allah amekupangia_* 



(❹) *_Ushukuru_*


→ unatakiwa umshukuru Allah kwa icho ambacho kimetokea au kukupata , hakika mtume wa Allah anapoona kitu ambacho hakimpendezi husema kuwa anamshukuru Allah kwa kila hali 


الحمد لله على كل حال 


{ sahihi jaami : 4640 } 


Kwaio tunatakiwa tumshukuru Allah na Allah atatulipa thawabu na lililobora kuliko hilo ambalo limetukuta.


_____


QURAN NA SUNNAH TZ 

WHATSAPP NO +255713849566 


TEMBELEA KWENYE MITANDAO KWA MASOMO MENGINE ZAIDI👇🏾


websites.

http://qurannasunnahtz.blogspot.com/


Facebook page.

https://m.facebook.com/Quran-na-sunnah-tz-100238655597178/?ref=bookmarks


Instagram.

http://www.instagram.com/qurannasunnah


Whatsapp.

https://chat.whatsapp.com/FfEoBrL4bmr0vbNQhNPKFE


telegram.

https://t.me/joinchat/3WW1yKOS9-MzN2Zk


YouTube

http://m.youtube.com/channel/UC1i0tOe8KZP7L0-rOisIb2A



 

No comments

Powered by Blogger.